Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yaonya madaktari
Afya

Serikali yaonya madaktari

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

MADAKTARI nchini wamepigwa marufuku kuandika dawa za wagonjwa kwa kutumia majina ya kampuni kwa kuwa kitendo hicho kinasababisha baadhi ya wagonjwa kukosa dawa.Anaripoti Mwandishi Wetu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 10 Oktoba 2018 na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Faustine Ndugulile, ambapo amesema kuwa, kitendo cha baadhi ya madaktari kuandika dawa kwa kutumia majina ya kampuni kinasababisha wagonjwa kushindwa kununua baadhi ya dawa zinazotengenezwa katika kampuni nyingine.

“Madaktari wawaandikie wagonjwa dawa kwa majina ya asili kwa sababu ukimwandikia mgonjwa panado ni kumtaka lazima anunue dawa hiyo hata kama kuna dawa nyingine hawezi kupewa,” ameeleza Dk. Ndugulile.

Dk. Ndugulile amewataka madaktari nchini kuwaandikia dawa wagonjwa kwa kutumia majina ya kitaalamu ili kuwawezesha wagonjwa kupata urahisi wa kununua dawa zenye uwezo wa kutibu maradhi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!