Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yaonya madaktari
Afya

Serikali yaonya madaktari

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

MADAKTARI nchini wamepigwa marufuku kuandika dawa za wagonjwa kwa kutumia majina ya kampuni kwa kuwa kitendo hicho kinasababisha baadhi ya wagonjwa kukosa dawa.Anaripoti Mwandishi Wetu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 10 Oktoba 2018 na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Faustine Ndugulile, ambapo amesema kuwa, kitendo cha baadhi ya madaktari kuandika dawa kwa kutumia majina ya kampuni kinasababisha wagonjwa kushindwa kununua baadhi ya dawa zinazotengenezwa katika kampuni nyingine.

“Madaktari wawaandikie wagonjwa dawa kwa majina ya asili kwa sababu ukimwandikia mgonjwa panado ni kumtaka lazima anunue dawa hiyo hata kama kuna dawa nyingine hawezi kupewa,” ameeleza Dk. Ndugulile.

Dk. Ndugulile amewataka madaktari nchini kuwaandikia dawa wagonjwa kwa kutumia majina ya kitaalamu ili kuwawezesha wagonjwa kupata urahisi wa kununua dawa zenye uwezo wa kutibu maradhi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

error: Content is protected !!