Thursday , 23 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo wa vyama siasa wajifungia Dar kujadili Demokrasia
Habari za SiasaTangulizi

Vigogo wa vyama siasa wajifungia Dar kujadili Demokrasia

Spread the love

BAADHI ya viongozi waandamizi wa vyama vya siasa hapa nchini leo tarehe 10 Oktoba 2018 wamekutana katika mkutano maalum unaoendelea kwenye hoteli ya New Afrika iliyoko jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Mkutano huo maalum kwa ajili ya kujadili kuhusu demokrasia hapa nchini, umeandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kuwezeshwa na Taasisi ya Kujenga Azaki za kijamii Tanzania (FCSTZ).

Viongozi wa vyama vya siasa waliohudhuria katika mkutano huo ni pamoja na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Yeremia Maganja, pamoja na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CUF, Juma Duni Hajji.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini, kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa, mkutano huo ni mwanzo wa mjadala wa kitaifa kuhusu demokrasia kutokana na vyama vikuu vya siasa kutuma uwakilishi mkubwa.

“Mkutano Maalumu wa Viongozi wa vyama vya Siasa ulioandaliwa na @MwalimuNyerere Foundation na kuwezeshwa na @FCSTZ unaendelea hapa Hoteli ya New Afrika.Vyama vyote vikuu vimetuma uwakilishi mkubwa.Huu waweza kuwa mwanzo wa mjadala wa kitaifa kuhusu Demokrasia yetu @Twaweza_NiSisi,” ameandika Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!