Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo wa vyama siasa wajifungia Dar kujadili Demokrasia
Habari za SiasaTangulizi

Vigogo wa vyama siasa wajifungia Dar kujadili Demokrasia

Spread the love

BAADHI ya viongozi waandamizi wa vyama vya siasa hapa nchini leo tarehe 10 Oktoba 2018 wamekutana katika mkutano maalum unaoendelea kwenye hoteli ya New Afrika iliyoko jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Mkutano huo maalum kwa ajili ya kujadili kuhusu demokrasia hapa nchini, umeandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kuwezeshwa na Taasisi ya Kujenga Azaki za kijamii Tanzania (FCSTZ).

Viongozi wa vyama vya siasa waliohudhuria katika mkutano huo ni pamoja na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Yeremia Maganja, pamoja na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CUF, Juma Duni Hajji.

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini, kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa, mkutano huo ni mwanzo wa mjadala wa kitaifa kuhusu demokrasia kutokana na vyama vikuu vya siasa kutuma uwakilishi mkubwa.

“Mkutano Maalumu wa Viongozi wa vyama vya Siasa ulioandaliwa na @MwalimuNyerere Foundation na kuwezeshwa na @FCSTZ unaendelea hapa Hoteli ya New Afrika.Vyama vyote vikuu vimetuma uwakilishi mkubwa.Huu waweza kuwa mwanzo wa mjadala wa kitaifa kuhusu Demokrasia yetu @Twaweza_NiSisi,” ameandika Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!