Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal
Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Bassirou Diomaye Faye
Spread the love

RAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa upinzani, Bassirou Diomaye Faye, kwa kufanikiwa kushinda kiti cha urais wa Senegal, katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametuma pongezi hizo leo tarehe 27 Machi 2024, kupitia ukurasa wake wa Twitter.

“Nawasilisha pongezi zangu za dhati kwa mheshimiwa Faye, Rais mteule wa Jamhuri ya Senegal kwa ushindi wako katika uchaguzi wa urais wa 2024 na watu kwa uchaguzi wa amani. Una matakwa yangu bora, natarajia kuendelea kufanya kazi pamoja ili kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Senegal,” ameandika.

Faye mwenye umri wa miaka 44, alitangazwa mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni baada ya kupata asilimia 53.7 ya kura huku mgombea wa chama tawala nchini humo, Amadou Ba (62) akipata asilimia 36.2.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu, Halima Mdee hapatoshi

Spread the loveVITA ya maneno kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

error: Content is protected !!