Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bihimba awavunjia ukimya wanaharakati
Habari Mchanganyiko

Bihimba awavunjia ukimya wanaharakati

Spread the love

MWANAHARAKATI huru, Bihimba Mpaya, amewataka wanaharakati kujikita zaidi katika kuisaidia jamii na kuwataka baadhi yao ambao wanatumia majukwaa yao vibaya kuacha mara moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Bihimba alitoa wito huo jana tarehe 26 Machi 2024, wakati akitoa msaada wa kiasi cha Sh. 200,000 kwa vikundi vya wajasiriamali wadogo wadogo Tanzania (SHIVUTA) na Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI), katika hafla ya harambee ya kutafuta fedha za kununua mabasi ya kusafirisha abiria (kosta) tano.

Amedai wapo baadhi ya wanaharakati wanatumia majukwaa yao vibaya kutoa lugha za uchochezi na kusahau majukumu yao ya kuisaidia jamii.

“Kuna uanaharakati wa aina nyingi, kuna wengine wanaharakati wa kufokafoka lakini mimi ninasaidia jamii. Uanaharakati huu nimejifunza kwa Martin Luther King, alikuwa anafanya harakati za kuisaidia jamii,” alisema Bihimba.

Bihimba alisema mara kwa mara amekuwa akitumia fedha zake anazopata kupitia kampuni yake ya usafirishaji ya Bihimba Tudo Transport, kuisaidia jamii kwa kuwa anatambua umuhimu wa kusaidia makundi ya watu wenye uhitaji.

Mwanaharakati huyo amekuwa akitoa msaada kwa wananchi wenye uhitaji hususan wa Jimbo la Ukonga, ambapo ameshawahi kuchangia ujenzi wa baadhi ya shule za sekondari za umma, misikiti na madrasa. Pamoja na kusaidia watu wenye mahitaji maalum kama walemavu na wajane.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!