Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa afariki dunia, magonjwa 3 yatajwa
Habari za SiasaTangulizi

Lowassa afariki dunia, magonjwa 3 yatajwa

Spread the love

Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Edward Lowassa (70) amefariki Dunia leo tarehe 10 Februari 2024 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Jijini (JKCI) Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akitangaza kifo hicho kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan kupitia televisheni ya Taifa (TBC), Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango amesema Lowassa amefariki leo saa nane mchana.

Amesema Lowassa amefariki katika hospitali hiyo ya JKCI alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa kujikunja utumbo, matatizo ya mapafu na shinikizo la  damu.

“Lowassa ameugua kwa muda mrefu, amekuwa akipatiwa matibabu tangu tarehe 14 Januari 2022 katika hospitali ya JKCI na baadae Afrika kusini na kurejea JKCI.

“Rais Samia aanatoa polea kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu mkubwa pia ametangaza siku tano za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa,” amesema Dk. Mpango.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!