Friday , 10 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Uingereza yatahadharisha raia wake Uganda
Kimataifa

Uingereza yatahadharisha raia wake Uganda

Spread the love

Serikali ya Uingereza imetoa tahadhari kwa raia wake wajiepushe kuitembelea mbuga mashuhuri ya wanyama nchini Uganda ambako watalii wawili, akiwemo raia mmoja wa Uingereza, wameuawa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Maafisa wa polisi na wa mbuga ya wanyama wamesema watu hao watatu walishambuliwa jana Jumanne na watu waliokuwa na bunduki wakati walipokuwa wakifanya safari katika mbuga ya kitaifa ya Malkia Elizabeth kusini magharibi mwa Uganda na gari yao kutiwa moto.

Shirika la Huduma za Wanyamapori la Uganda limewatambua wahanga wengine wawili kama mtalii wa Afrika Kusini na muongozaji safari wa Uganda.

Polisi wamelinyooshea kidole cha lawama kundi la Allied Democratic Forces (ADF) kwa shambulizi hilo.

Msemaji wa polisi, Fred Enanga amesema vikosi vyao vya pamoja vilichukua hatua mara tu baada ya kupokea taarifa na wanawasaka washukiwa waasi wa kundi la ADF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!