Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais awatimua mawaziri kwa kuchelewa kikaoni
KimataifaTangulizi

Rais awatimua mawaziri kwa kuchelewa kikaoni

Dk. Wiliam Ruto
Spread the love

RAIS wa Kenya, William Ruto amemtimua Waziri wa Biashara, Moses Kuria na mwenzake wa Usalama wa Ndani Kithuri Kindiki baada ya kuchelewa kwenye hafla ya utiaji saini mikataba ya zabuni mbalimbali iliyofanyika ikulu jijini Nairobi. Anaripoti Mlelwa Kiwale, Tudarco … (endelea).  

Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 1 Agosti 2023, ambapo imeelezwa kuwa  Rais Ruto aliwahi kufika kwenye ukumbi uliopangwa kufanyika shughuli hiyo kabla ya mawaziri hao ndipo alipoamua kufunga mlango.

Kiongozi huyo mkuu wa Kenya amesema mawaziri hao watalazimika kujieleza juu ya kitendo hicho kwa njia ya maandishi.

 “Kwa hiyo wale ambao waliochelewa ambao ni watumishi na watendaji waandamizi, nategemea kupata maelezo kwa maandishi.  Licha ya kudai kuwa wamechelewa sababu ya foleni nataka kufahamu kwanini hawaichukulii hii hafla ya utiaji saini mikataba kwa umakini”.

Aidha, Rais Ruto ametoa tahadhari kwa watumishi wengine wa umma kuacha kubeza shughuli hizo kwa kuona kuwa hazina msingi kwenye utendaji serikali.

Ruto alionesha kukasirishwa na kusema kuwa inaonekana wafanyakazi wa serikali yake wanaichukulia hafla hiyo kama  ibada.

“Sijajua kwamba sababu ya hii usainishaji wa mikataba uliokuwa ukiendendelea takribani miaka 20 sasa watu wanafikiria kwamba ni ibada”

“Ndiyo maana watu wanachukulia kama kitu cha zamani na kuleta samahani zisizo za maana” amesisitiza Ruto.

Ruto amesema mtumishi wa  serikali ambaye hakuzingatia muda anatakiwa kujiuzulu mwenyewe.

“Kama hautoweza kuzingatia muda kwa muajiri wako, basi unatakiwa kujiuzulu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu, Halima Mdee hapatoshi

Spread the loveVITA ya maneno kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha...

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamkaba koo Mo Dewji kwa kutelekeza viwanda vya chai

Spread the loveSERIKALI inakusudia kumuweka kikaangoni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mohammed Enterprises...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

error: Content is protected !!