RAIS wa Kenya, William Ruto amemtimua Waziri wa Biashara, Moses Kuria na mwenzake wa Usalama wa Ndani Kithuri Kindiki baada ya kuchelewa kwenye hafla ya utiaji saini mikataba ya zabuni mbalimbali iliyofanyika ikulu jijini Nairobi. Anaripoti Mlelwa Kiwale, Tudarco … (endelea).
Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 1 Agosti 2023, ambapo imeelezwa kuwa Rais Ruto aliwahi kufika kwenye ukumbi uliopangwa kufanyika shughuli hiyo kabla ya mawaziri hao ndipo alipoamua kufunga mlango.
Kiongozi huyo mkuu wa Kenya amesema mawaziri hao watalazimika kujieleza juu ya kitendo hicho kwa njia ya maandishi.
“Kwa hiyo wale ambao waliochelewa ambao ni watumishi na watendaji waandamizi, nategemea kupata maelezo kwa maandishi. Licha ya kudai kuwa wamechelewa sababu ya foleni nataka kufahamu kwanini hawaichukulii hii hafla ya utiaji saini mikataba kwa umakini”.
Aidha, Rais Ruto ametoa tahadhari kwa watumishi wengine wa umma kuacha kubeza shughuli hizo kwa kuona kuwa hazina msingi kwenye utendaji serikali.
Ruto alionesha kukasirishwa na kusema kuwa inaonekana wafanyakazi wa serikali yake wanaichukulia hafla hiyo kama ibada.
“Sijajua kwamba sababu ya hii usainishaji wa mikataba uliokuwa ukiendendelea takribani miaka 20 sasa watu wanafikiria kwamba ni ibada”
“Ndiyo maana watu wanachukulia kama kitu cha zamani na kuleta samahani zisizo za maana” amesisitiza Ruto.
Ruto amesema mtumishi wa serikali ambaye hakuzingatia muda anatakiwa kujiuzulu mwenyewe.
“Kama hautoweza kuzingatia muda kwa muajiri wako, basi unatakiwa kujiuzulu,” amesema.
Leave a comment