Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima
Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the love

MSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga umepita katika eneo la Kawangware jijini Nairobi nchini Kenya na kupata fursa ya kuwahutubia wakazi hao lakini baada ya muda mfupi, wafuasi wake wakatimuliwa kwa mabomu ya machozi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

“Sisi wana-Azimio tunasema gharama ya maisha zishuke, bei ya unga irudi chini, bei ya mafuta irudi chini, sukari irudi chini na ‘server’ ifunguliwe,” amesema Raila kwenye msafara huo.

Viongozi walioandamana na Raila ni Martha Karua, Eugene Wamalwa, Wycliffe Oparanya, Jeremiah Kioni na kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka, kiongozi wa chama cha Roots Party George Wajackoyah na miongoni mwa viongozi wengine.

Wakati akiendelea na maandamano hay oleo tarehe 27 Machi 2023, Odinga dakika chache baada ya kuanzisha maandamno hayo huku msafara wa kiongozi huyo ukipenya katika makazi hayo, maofisa wa polisi waliwarushia mabomu ya machozi waandamanaji waliokuwa wamebeba matawi ya miti, mabango, sufuria na baadhi ya vyakula ili kupinga hali ya juu ya maisha.

Hatua hiyo inajiri baada ya Inspekta mkuu wa Polisi IGP nchini humo, kudai kwamba maandamano hayo yalikuwa haramu.

Haya yanajiri huku genge la vijana likivamia shamba la Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta lililoko Eastern Bypass. Dhamira ya watu hao haijabainika kufikia sasa.

Kenyatta alimuunga mkono Raila kwenye uchaguzi mkuu wa tarehe 9 Agosti 2022.

Serikali ya Kenya inayoongozwa na Rais William Ruto inalaumiwa kwa kile upinzani inachodai kuwa ni kuwanyanyasa raia kwa kusababisha ongezeko la gharama za maisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!