Friday , 10 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu
Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love

 

KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu atavaa viatu vyake vya uongozi pindi itakapotokea akafariki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tunduru … (endelea).

Amesema malengo ya chama hicho ni kushika dola hivyo kwa hatua waliyofikia na namna alivyomuandaa Ado ana uhakika kuwa atakiongoza chama hicho kuchukua madaraka.

Zitto ametoa kauli hiyo jana tarehe 13 Machi 2023 wakati akihutubia wananchi wa Tunduru mkoani Ruvuma katika mkutano wa hadhara.

Amesema; “Mimi ni kiongozi wa chama hiki, nina matamanio ya kuona nakipeleka chama kushika dola, lakini Mwenyezi Mungu naye ana mipango yake.

“Hata ikitokea leo Mwenyezi Mungu amesema bwana siku zako zimefika sasa nakuita, nitakwenda kwenye nyumba yangu ya milele nikiwa natabasamu,” amesema.

Amesema atakwenda akiwa anaamini kwamba ameacha mtu atakayeendeleza mapambano kama ambavyo Oliver Tambo alivyomuachia Nelson Mandela –(Afrika Kusini) au kama ambavyo Eduardo Mondlane alivyomuachia Samora Machel (Msumbiji) na huyo mtu ni Ado Shaibu.

Amewaomba wananchi hao kuwa ACT Wazalendo kiwe chama chao na sio suala la mjadala kufanya uamuzi tena.

Amesema chama hicho ndio chama kilichowathamini wana Tunduru kwa kumshika mkono mtoto wao (Ado) na kumpa majukumu mazito.

“Sasa nasema hata Mwenyezi Mumgu akinichukua sina wasiwasi… Ado atavaa viatu vyangu, ataendeleza mapambano mpaka tutakaposhika madaraka,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!