Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko BoT yaongeza siku 30 usimamizi wa Yetu Microfinance Bank Plc
Habari Mchanganyiko

BoT yaongeza siku 30 usimamizi wa Yetu Microfinance Bank Plc

Spread the love

 

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeongeza muda wa siku 30 wa usimamizi wa Yetu Microfinance Bank Plc baada ya mchakato wa kutathmini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa matatizo ya taasisi hiyo ya kifedha kutokamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hatua hiyo inakuja baada ya tarehe 12 Disemba 2022 BoT kusitisha shughuli za utoaji wa huduma za kibenki za Yetu Microfinance Bank Plc kwa muda wa siku 90 ili kuipa nafasi Benki Kuu ya Tanzania kutathmini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa suala hili.

Hata hivyo katika taarifa iliyotolewa leo tarehe 14 Machi 2023 na Gavana wa BoT, Emanuel Tutuba imesema muda wa usimamizi umeongezwa kwa kipindi cha siku 30 kuanzia tarehe 12 Machi 2023.

“Itakumbukwa kwamba, kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha sheria namba 56(1)(g)(iii) cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Benki Kuu ya Tanzania iliamua kuchukua usimamizi wa Yetu Microfinance Bank Plc kuanzia tarehe 12 Disemba 2022 baada ya kubaini kuwa ilikuwa na upungufu mkubwa wa ukwasi na mtaji kinyume na matakwa ya sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006 na kanuni zake.

“Baada ya kuchukua usimamizi wa benki hii, Benki Kuu ya Tanzania ilisitisha shughuli za utoaji wa huduma za kibenki za Yetu Microfinance Bank Plc kwa muda wa siku 90 ili kuipa nafasi Benki Kuu ya Tanzania kutathmini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa suala hili,” imesema taarifa hiyo.

Aidha, BoT imeuhakikishia umma kuwa itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!