Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kimbunga Freddy chaua 100 Malawi, Msumbiji
Kimataifa

Kimbunga Freddy chaua 100 Malawi, Msumbiji

Moja ya athari zilizotokea kutokana na KImbunga Freddy
Spread the love

 

KIMBUNGA Freddy, kilichoambatana na upepo mkali na mvua kubwa, kimerejea kusini mwa Afrika na kuua watu takriban 100 katika nchi za Malawi na Msumbiji. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kimbunga Freddy, kinachoelekea kuwa dhoruba ya muda mrefu iliyovunja rekodi ya kudumu, kilipiga sehemu za kusini mwa Afrika mwisho mwa wiki kwa mara ya pili ndani ya wiki chache, na kurejea tena baada ya mara kwanza kupiga katika eneo hilo mwishoni mwa mwezi.

Kimbunga hicho kililikumba eneo la kati la Msumbiji siku ya Jumamosi, na kuezua paa za majengo na kuleta mafuriko kuzunguka bandari ya Quelimane, kabla ya kuingia ndani kuelekea Malawi na mvua kubwa iliyosababisha maporomoko ya ardhi.

Kiwango kamili cha uharibifu na upotezaji wa maisha nchini Msumbiji bado hakijabainika, kwani umeme na simu zimekatika katika baadhi ya maeneo yalioathiriwa.

Dharuba hiyo imeua watu 99 nchini Malawi, wakiwemo 85 katika kituo kikuu cha kibiashara cha Blantyre, alisema kamishna wa Idara ya Masuala ya Kukabiliana na Maafa, Charles Kalemba, katika mkutano na waandishi wa habari.

Rais wa nchi hiyo Lazarus Chakwera alitangaza hali ya hatari katika eneo la Kusini mwa nchi hiyo baada ya kuelezea wasiwasi mkubwa kuhusu uharibifu uliosababishwa na kimbunga Freddy.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!