KIMBUNGA Freddy, kilichoambatana na upepo mkali na mvua kubwa, kimerejea kusini mwa Afrika na kuua watu takriban 100 katika nchi za Malawi na Msumbiji. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Kimbunga Freddy, kinachoelekea kuwa dhoruba ya muda mrefu iliyovunja rekodi ya kudumu, kilipiga sehemu za kusini mwa Afrika mwisho mwa wiki kwa mara ya pili ndani ya wiki chache, na kurejea tena baada ya mara kwanza kupiga katika eneo hilo mwishoni mwa mwezi.
Kimbunga hicho kililikumba eneo la kati la Msumbiji siku ya Jumamosi, na kuezua paa za majengo na kuleta mafuriko kuzunguka bandari ya Quelimane, kabla ya kuingia ndani kuelekea Malawi na mvua kubwa iliyosababisha maporomoko ya ardhi.
Kiwango kamili cha uharibifu na upotezaji wa maisha nchini Msumbiji bado hakijabainika, kwani umeme na simu zimekatika katika baadhi ya maeneo yalioathiriwa.
Dharuba hiyo imeua watu 99 nchini Malawi, wakiwemo 85 katika kituo kikuu cha kibiashara cha Blantyre, alisema kamishna wa Idara ya Masuala ya Kukabiliana na Maafa, Charles Kalemba, katika mkutano na waandishi wa habari.
Rais wa nchi hiyo Lazarus Chakwera alitangaza hali ya hatari katika eneo la Kusini mwa nchi hiyo baada ya kuelezea wasiwasi mkubwa kuhusu uharibifu uliosababishwa na kimbunga Freddy.
Leave a comment