Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu
Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love

 

KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu atavaa viatu vyake vya uongozi pindi itakapotokea akafariki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tunduru … (endelea).

Amesema malengo ya chama hicho ni kushika dola hivyo kwa hatua waliyofikia na namna alivyomuandaa Ado ana uhakika kuwa atakiongoza chama hicho kuchukua madaraka.

Zitto ametoa kauli hiyo jana tarehe 13 Machi 2023 wakati akihutubia wananchi wa Tunduru mkoani Ruvuma katika mkutano wa hadhara.

Amesema; “Mimi ni kiongozi wa chama hiki, nina matamanio ya kuona nakipeleka chama kushika dola, lakini Mwenyezi Mungu naye ana mipango yake.

“Hata ikitokea leo Mwenyezi Mungu amesema bwana siku zako zimefika sasa nakuita, nitakwenda kwenye nyumba yangu ya milele nikiwa natabasamu,” amesema.

Amesema atakwenda akiwa anaamini kwamba ameacha mtu atakayeendeleza mapambano kama ambavyo Oliver Tambo alivyomuachia Nelson Mandela –(Afrika Kusini) au kama ambavyo Eduardo Mondlane alivyomuachia Samora Machel (Msumbiji) na huyo mtu ni Ado Shaibu.

Amewaomba wananchi hao kuwa ACT Wazalendo kiwe chama chao na sio suala la mjadala kufanya uamuzi tena.

Amesema chama hicho ndio chama kilichowathamini wana Tunduru kwa kumshika mkono mtoto wao (Ado) na kumpa majukumu mazito.

“Sasa nasema hata Mwenyezi Mumgu akinichukua sina wasiwasi… Ado atavaa viatu vyangu, ataendeleza mapambano mpaka tutakaposhika madaraka,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!