Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino
Kimataifa

Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino

Rais wa Ufilipino, Fedinard Marcos
Spread the love

 

ROEL Degamo (56), Gavana wa jimbo la katikati mwa Ufilipino pamoja na watu wengine watano, wameuawa jana Jumamosi, tarahe 4 Machi, kwa kufyatuliwa risasi na watu wasiojulikana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Hili ni shambulio la hivi punde dhidi ya maafisa wa serikali. Degamo, alikuwa gavana wa jimbo la Negros Oriental.

Polisi wamesema washukiwa sita waliokuwa wamebeba bunduki na waliovalia sare zinazofanana na zile zinazovaliwa na wanajeshi, waliingia katika nyumba ya gavana huyo aliyekuwa akitoa msaada kwa wananchi katika mji wa Pamplona na kuanza kufyatua risasi.

Rais wa Ufilipino, Ferdinand Marcos amelaani kile alichokitaja kuwa ni “mauaji” ya mshirika wake wa kisiasa.

Ameahidi kuwafikisha wahusika wa uhalifu huo mbele ya vyombo vya sheria.

Takriban wanasiasa watatu wameuawa kwa risasi tangu uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!