Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Geita apiga stop MA-DC kuwaweka watumishi mahabusu, “ni ushamba”
Habari Mchanganyiko

RC Geita apiga stop MA-DC kuwaweka watumishi mahabusu, “ni ushamba”

Spread the love

 

MKUU wa mkoa wa Geita, Martin Shigella amesema amekubaliana na wakuu wa wilaya za mkoa huo kwamba hakuna mtumishi yeyote atakayekamatwa na kuwekwa ndani kwa sababu za kinidhamu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea).

Pia amesema tangu ahamishiwe kushika wadhifa huo katika mkoa wa Geita, hajapokea malalamiko yoyote kutoka kwa wananchi, watumishi au viongozi kuhusu utendaji wa wakurugenzi au Baraza la Madiwani wa halmashauri za mkoa huo.

Shigella ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Machi 2023 katika mdahalo wa kujadili miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita madarakani chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema mtumishi anaweza kukamatwa na kufikishwa polisi iwapo atakuwa ametenda kosa la jinai lakini si katika masuala ya nidhamu.

Ametoa mfano kwamba mwalimu anaweza kuchelewa kikao kilichoitishwa na mkuu wa wilaya kwa sababu mwanaye ameumwa ghafla hivyo jambo kama hilo halipaswi kuchukuliwa kimabavu na mkuu wa wilaya kwa kumuweka mwalimu huyo ndani kisha kachelewa kikao.

“Kumuweka mwalimu mahabusu saa 48 kwa sababu ya kuchelewa kikao ni jambo la kishamba, hili halina nafasi kwenye mkoa wetu.

“Hayo ndio maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan, alituelekeza sisi wakuu wa mikoa. Niwahakikishie hutasikia hilo jambo kwa sababu tuna kazi kubwa ya kufanya si kuja kugombana.

“Niwahakikishie hutasikia hilo jambo kwa sababu tuna kazi kubwa ya kufanya si kuja kugombana hizi nafasi ni dhamana tu,” amesema.

Aidha, amesema ana miezi sita ya uongozi kwenye mkoa, lakini hajapata malalamiko kuwahusu wakurugenzi au viiongozi wengine wa mkoa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!