Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino
Kimataifa

Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino

Rais wa Ufilipino, Fedinard Marcos
Spread the love

 

ROEL Degamo (56), Gavana wa jimbo la katikati mwa Ufilipino pamoja na watu wengine watano, wameuawa jana Jumamosi, tarahe 4 Machi, kwa kufyatuliwa risasi na watu wasiojulikana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Hili ni shambulio la hivi punde dhidi ya maafisa wa serikali. Degamo, alikuwa gavana wa jimbo la Negros Oriental.

Polisi wamesema washukiwa sita waliokuwa wamebeba bunduki na waliovalia sare zinazofanana na zile zinazovaliwa na wanajeshi, waliingia katika nyumba ya gavana huyo aliyekuwa akitoa msaada kwa wananchi katika mji wa Pamplona na kuanza kufyatua risasi.

Rais wa Ufilipino, Ferdinand Marcos amelaani kile alichokitaja kuwa ni “mauaji” ya mshirika wake wa kisiasa.

Ameahidi kuwafikisha wahusika wa uhalifu huo mbele ya vyombo vya sheria.

Takriban wanasiasa watatu wameuawa kwa risasi tangu uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

Kimataifa

Netanyau asitisha mipango yenye utata marekebisho mfumo wa sheria

Spread the love  WAZIRI Mkuu wa nchini Israel, Benjamin Netanyahu amesema atachelewesha...

Kimataifa

Raila ahutubia waandamanaji, mabomu yarindima

Spread the loveMSAFARA wa kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

error: Content is protected !!