Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino
Kimataifa

Gavana na watu wengine 5 wauawa kwa risasi Ufilipino

Rais wa Ufilipino, Fedinard Marcos
Spread the love

 

ROEL Degamo (56), Gavana wa jimbo la katikati mwa Ufilipino pamoja na watu wengine watano, wameuawa jana Jumamosi, tarahe 4 Machi, kwa kufyatuliwa risasi na watu wasiojulikana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Hili ni shambulio la hivi punde dhidi ya maafisa wa serikali. Degamo, alikuwa gavana wa jimbo la Negros Oriental.

Polisi wamesema washukiwa sita waliokuwa wamebeba bunduki na waliovalia sare zinazofanana na zile zinazovaliwa na wanajeshi, waliingia katika nyumba ya gavana huyo aliyekuwa akitoa msaada kwa wananchi katika mji wa Pamplona na kuanza kufyatua risasi.

Rais wa Ufilipino, Ferdinand Marcos amelaani kile alichokitaja kuwa ni “mauaji” ya mshirika wake wa kisiasa.

Ameahidi kuwafikisha wahusika wa uhalifu huo mbele ya vyombo vya sheria.

Takriban wanasiasa watatu wameuawa kwa risasi tangu uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!