Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania inakabiliwa na uhaba wa nyumba milioni 3
Habari Mchanganyiko

Tanzania inakabiliwa na uhaba wa nyumba milioni 3

Spread the love

 

TANZANIA inakabiliwa na uhaba wa nyumba zipatazo milioni tatu licha ya kuwa watanzania ni zaidi ya milioni sitini ambapo jiji la Dar es salaam kuna uhaba wa nyumba laki nne. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Pamoja na kuwepo kwa upungufu wa nyumba imeelezwa kuwa ni asilimia 15 tu ya watanzania ambao wanaweza kumiliki nyumba ambazo thamani yake ni kuanzia Sh 25 milioni 25 na kuendelea.

Hayo yameelezwa leo tarehe 9 Februar 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investiments, Dk.Fred Msemwa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya maendeleo ya taasisi hiyo.

Aidha Dk.Msemwa ameeleza kuwa bado watanzania hawajaweza kuwa na utayari wa kuwekeza katika sekta ya pesa kwa maana kuwa hawawezi kununua hisa na amana na kupelekea kuwa ni watanzania laki 8 pekee wenye kushiriki katika kuwekeza katika biashara ya fedha.

Amesema kuwa ili kuweza kuwa na nyumba bora na za bei nafuu taasisi imeona ni vyema pia watanzania wakawa na elimu ya umuhimu wa uwekezaji katika sekata ya pesa.

“Watanzania lazima wajue kuwa kuna tofauti sana ya kuwa na fedha na kuwekeza katika katika sekta ya kifedha kwani kuwekeza katika fedha na kuwa na nyumba bora na yenye gharama nafuu ni mambo ambayo yanafanana,” ameeleza Dk Msemwa.

Aidha ameeleza kuwa jumla ya nyumba zimejengwa 983 zimejengwa katika mikoa 19 ya Tanzania bara huku nyumba za gharama nafuu zikiendelea kujengwa katika mikoa yenye uhaba wa nyumba za walimu,watumishi na kada mbalimbali wenye kipato cha chini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!