Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kisa video iliyomuumbua Rais akijisaidia haja ndogo hadharani, waandishi habari 6 mbaroni
Kimataifa

Kisa video iliyomuumbua Rais akijisaidia haja ndogo hadharani, waandishi habari 6 mbaroni

Spread the love

WAANDISHI habari kadhaa wamekamatwa nchini Sudan Kusini baada ya kusambaa video inayomuonesha Rais wa nchi hiyo Salva Kiir yumkini akishindwa kujizuia haja ndogo kwenye hafla rasmi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Jumuiya ya waandishi habari ya Sudan Kusini imetoa wito wa kufanyika uchunguzi haraka kuhusu tukio hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Video hiyo iliyotolewa na Shirika la Taifa la Utangazaji la Sudan imemwonesha Rais Kiir mwenye umri wa miaka 72 akilowesha suruali yake wakati wimbo wa taifa ukipigwa kwenye sherehe ya ufunguzi katika mji mkuu Juba mwezi uliopita.

Waandishi hao sita walikamatwa baada ya video husika kuanza kusambaa.

Waliotiwa mbaroni ni pamoja na mkurugenzi wa kitengo cha udhibiti, mhariri wa maudhui, wapiga picha kadhaa na mafundi waliokuwapo wakati rais huyo akipigwa picha.

Wizara ya habari imesema waandishi hao wanasaidia katika juhudi za uchunguzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!