Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Vincent Aboubakar ampisha Ronaldo Al-Nassr, anukia Man United
Michezo

Vincent Aboubakar ampisha Ronaldo Al-Nassr, anukia Man United

Spread the love

KLABU ya Al-Nassr inayoshiriki Ligi Kuu ya Saudi Arabia imesitisha mkataba wa mshambuliaji wa Cameroon, Vincent Aboubakar ili kumpisha straika mpya raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Kwa mujibu wa kanuni za ligi hiyo, klabu zinaruhusiwa kuwa na wachezaji wanane wasio raia wa Saudi Arabia.

Kabla ya ujio wa Ronaldo, Al-Nassr ilikuwa imefikisha idadi ya wachezaji wanaoruhusiwa kwa hivyo ilikuwa lazima mmoja wao angetimuliwa ili kutengeneza nafasi ya nyota huyo wa Ureno.

Kwa mujibu wa RMC Sport, mkataba wa Aboubakar ulivunjwa baada ya makubaliano ya pamoja na atapokea malipo ya mkataba huo. Sasa ni mchezaji huru.

Aboubakar amehusishwa na uhamisho kuelekea klabu ya Manchester United ambayo inazidi kuwinda mshambuliaji katika dirisha fupi la uhamisho.

Raia huyo wa Cameroon alitamba katika Kombe la Dunia akifunga bao la ushindi dhidi ya Brazil. Pia alifunga mabao 13 na kutoa pasi 6 za mabao katika mechi 39 akiwa na miamba ya Al-Nassr.

Kuondoka kwa nahodha huyo wa Cameroon kunaruhusu Ronaldo kuandikishwa na kuwa huru kuchezea klabu yake mpya – japo atasubiri zaidi kwani anatumikia marufuku ya mechi mbili aliyopigwa kwa kuvunja simu ya shabiki akiwa nchini Uingereza.

Ronaldo tayari alikosa mechi ya kwanza ambako Al-Nassr iliipiga Al-Ta’ee 2-0 akitazama katika eneo la wageni mashuhuri na pia atakosa mechi ya Jumamosi ijayo dhidi ya Al-Shabab. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United, Real Madrid na Juventus atakuwa huru kuchezea Al-Nassr tarehe 22 Januari, 2023 katika mechi yao ya nyumbani na Ettifaq.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!