WAANDISHI habari kadhaa wamekamatwa nchini Sudan Kusini baada ya kusambaa video inayomuonesha Rais wa nchi hiyo Salva Kiir yumkini akishindwa kujizuia haja ndogo kwenye hafla rasmi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Jumuiya ya waandishi habari ya Sudan Kusini imetoa wito wa kufanyika uchunguzi haraka kuhusu tukio hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Video hiyo iliyotolewa na Shirika la Taifa la Utangazaji la Sudan imemwonesha Rais Kiir mwenye umri wa miaka 72 akilowesha suruali yake wakati wimbo wa taifa ukipigwa kwenye sherehe ya ufunguzi katika mji mkuu Juba mwezi uliopita.
Waandishi hao sita walikamatwa baada ya video husika kuanza kusambaa.
Waliotiwa mbaroni ni pamoja na mkurugenzi wa kitengo cha udhibiti, mhariri wa maudhui, wapiga picha kadhaa na mafundi waliokuwapo wakati rais huyo akipigwa picha.
Wizara ya habari imesema waandishi hao wanasaidia katika juhudi za uchunguzi.
Leave a comment