Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Tumefarijika, tumeuanza mwaka mpya vizuri
Habari za Siasa

Zitto: Tumefarijika, tumeuanza mwaka mpya vizuri

Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)
Spread the love

 

KIONGOZI wa ACT Wazalendo, Zitto kabwe amesema wamefarijika sana baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza kufuta zuio la mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa.

Ameongeza kuwa ni dhahiri kwamba Watanzania wameuanza mwaka vizuri hasa ikizingatiwa suala la mikutano ya hadhara ni jambo ambalo walikuwa wakilizungumzia siku nyingi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Januari, 2023 Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kuhudhuria mkutano ulioitishwa na Rais Samia dhidi ya viongozi wa vyama 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu.

“Leo rais kama alivyokuwa ameahidi siku zote, ametembea kwenye maneno yake. Kwa hiyo ni hatua kubwa kwetu sisi ni furaha, ndio maana mmeona alivyotamka hiyo tulisimama kushangilia.

“Lakini michakato ya marekebisho ya sheria mbalimbali kama ambavyo imependekezwa na vyombo mbalimbali pia kukwamuliwa kwa mchakato wa katiba ni mambo muhimu, naamini sote kwa pamoja tutaweza kufanya kazi vizuri na kuimarisha demokrasia na ya nchi yetu. Nakumbuka haikuwa hali ya kawaida lakini sasa hivi tumefanikiwa na tutakutana kwenye majukwaa ya kisiasa,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!