Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: Tumefarijika, tumeuanza mwaka mpya vizuri
Habari za Siasa

Zitto: Tumefarijika, tumeuanza mwaka mpya vizuri

Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)
Spread the love

 

KIONGOZI wa ACT Wazalendo, Zitto kabwe amesema wamefarijika sana baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza kufuta zuio la mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa.

Ameongeza kuwa ni dhahiri kwamba Watanzania wameuanza mwaka vizuri hasa ikizingatiwa suala la mikutano ya hadhara ni jambo ambalo walikuwa wakilizungumzia siku nyingi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Januari, 2023 Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kuhudhuria mkutano ulioitishwa na Rais Samia dhidi ya viongozi wa vyama 19 vya siasa vyenye usajili wa kudumu.

“Leo rais kama alivyokuwa ameahidi siku zote, ametembea kwenye maneno yake. Kwa hiyo ni hatua kubwa kwetu sisi ni furaha, ndio maana mmeona alivyotamka hiyo tulisimama kushangilia.

“Lakini michakato ya marekebisho ya sheria mbalimbali kama ambavyo imependekezwa na vyombo mbalimbali pia kukwamuliwa kwa mchakato wa katiba ni mambo muhimu, naamini sote kwa pamoja tutaweza kufanya kazi vizuri na kuimarisha demokrasia na ya nchi yetu. Nakumbuka haikuwa hali ya kawaida lakini sasa hivi tumefanikiwa na tutakutana kwenye majukwaa ya kisiasa,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!