Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia amlilia balozi aliyefariki ajalini
HabariTangulizi

Rais Samia amlilia balozi aliyefariki ajalini

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Balozi wa Tanzania nchini Austria, Celestine Mushy, kilichotokea katika ajali ya gari iliyotokea usiku wa Jumanne, maeneo ya Mkata, wilayani Handeni, Mkoa wa Tanga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Dk. Samia ametuma salamu hizo za rambirambi leo Alhamisi, tarehe 15 Desemba 2022, kupitia ukurasa wake wa Twitter.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Balozi Celestine Mushy Balozi wa Tanzania nchini Austria na Mwakilishi wa Kudumu wa nchi yetu katika Mashirika ya Kimataifa, Vienna. Tumeondokewa na mwanadiplomasia mahiri na mtumishi makini wa umma. Mungu amweke mahali pema. Amina,” ameandika Rais Samia.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Siriel Mchembe, Balozi Mushy alifariki dunia akiwa safarini kuelekea mkoani Kilimanjaro, akitokea jijini Dar es Salaam.

Marehemu Balozi Mushy aliteuliwa na Rais Samia kuiwakilisha Tanzania nchini Austria, Januari 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!