RAIS Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Balozi wa Tanzania nchini Austria, Celestine Mushy, kilichotokea katika ajali ya gari iliyotokea usiku wa Jumanne, maeneo ya Mkata, wilayani Handeni, Mkoa wa Tanga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Dk. Samia ametuma salamu hizo za rambirambi leo Alhamisi, tarehe 15 Desemba 2022, kupitia ukurasa wake wa Twitter.
“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Balozi Celestine Mushy Balozi wa Tanzania nchini Austria na Mwakilishi wa Kudumu wa nchi yetu katika Mashirika ya Kimataifa, Vienna. Tumeondokewa na mwanadiplomasia mahiri na mtumishi makini wa umma. Mungu amweke mahali pema. Amina,” ameandika Rais Samia.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Siriel Mchembe, Balozi Mushy alifariki dunia akiwa safarini kuelekea mkoani Kilimanjaro, akitokea jijini Dar es Salaam.
Marehemu Balozi Mushy aliteuliwa na Rais Samia kuiwakilisha Tanzania nchini Austria, Januari 2022.
Leave a comment