Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba amng’oa kigogo CUF
Habari za Siasa

Prof. Lipumba amng’oa kigogo CUF

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera wa chama hicho, Habibu Mnyaa, huku sababu ikitajwa kuwa ni masuala ya uwajibikaji na nidhamu ndani ya chama hicho. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya utenguzi huo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 24 Novemba 2022 na Prof. Lipumba.

Taarifa ya Prof. Lipumba imesema, uteuzi wa kujaza nafasi hiyo utafanyika hivi karibuni.

“Tarehe 28 Aprili 2019 nilimteua Mohamed Habibu Mnyaa, kuwa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera na alithibitishwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa. Kwa kuzingatia uwajibikaji na nidhamu ndani ya Chama,” imesema taarifa ya Prof. Lipumba na kuongeza:

“Leo tarehe 24 Novemba 2022, natengua uteuzi wa Mohamed Habibu Mnyaa nafasi ya Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera.Uteuzi wa kujaza nafasi hiyo utafanyika baadaye na kuwasilishwa katika Kikao kijacho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!