Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba amng’oa kigogo CUF
Habari za Siasa

Prof. Lipumba amng’oa kigogo CUF

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera wa chama hicho, Habibu Mnyaa, huku sababu ikitajwa kuwa ni masuala ya uwajibikaji na nidhamu ndani ya chama hicho. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya utenguzi huo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 24 Novemba 2022 na Prof. Lipumba.

Taarifa ya Prof. Lipumba imesema, uteuzi wa kujaza nafasi hiyo utafanyika hivi karibuni.

“Tarehe 28 Aprili 2019 nilimteua Mohamed Habibu Mnyaa, kuwa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera na alithibitishwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa. Kwa kuzingatia uwajibikaji na nidhamu ndani ya Chama,” imesema taarifa ya Prof. Lipumba na kuongeza:

“Leo tarehe 24 Novemba 2022, natengua uteuzi wa Mohamed Habibu Mnyaa nafasi ya Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Bunge na Sera.Uteuzi wa kujaza nafasi hiyo utafanyika baadaye na kuwasilishwa katika Kikao kijacho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!