Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rwanda wadai kumuua mwanajeshi wa DRC
Kimataifa

Rwanda wadai kumuua mwanajeshi wa DRC

Spread the love

JESHI la Rwanda limedai kumuua mtu anayeaminiwa kuwa mwanajeshi kutoka nchi jirani ya DRC, katika Wilaya iliyopo mpakani ya Rubavu.

Tukio hilo limejiri huku uhusiano kati ya nchi hizo mbili ukizidi kutetereka kutokana na Congo kuituhumu Rwanda kuunga mkono waasi wa M23 wanaoitesa nchi hiyo. Anaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Ripoti iliyotolewa na jeshi la Rwanda inasema mtu huyo aliyekuwa amevalia magwanda ya jeshi la DRC na ambaye hakutambuliwa mara moja, anaamiwa kuwa mwanajeshi wa FARDC.

Aidha, jeshi la Rwanda linasema mtu huyo alivuka kizuizi cha “Petite Barrière” na kuanza kuwafyatulia risasi maafisa wa usalama, wakati alipopigwa risasi na mwanajeshi wa nchi yake kuepusha madhara zaidi.

Afisa wa DRC ambaye alikuwa katika eneo la tukio na kutotaka kufahamika amesema hakuna mwanajeshi wa DRC aliyekuwa anaweka doria katika eneo hilo la mpaka, licha ya makabiliano ya risasi kusikika usiku kucha.

Tukio hili limetokea baada ya mapema mwezi huu, ndege ya kivita ya DRC kuvuka mpaka wa anga bila ya idhini na kutua katika uwanja wa ndege wa Rubavu na kuikasirisha Rwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!