Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kiwanda cha iphone China chatoa ahadi ya kudhibiti Uviko 19
Habari Mchanganyiko

Kiwanda cha iphone China chatoa ahadi ya kudhibiti Uviko 19

Spread the love

 

KIWANDA cha Iphone cha Zhengzhou, China kimetoa ahadi ya kuhakikisha usalama kwa wafanyakazi walioamua kuondoka na wale watakaobaki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kiwanda hicho kimefikia uamuzi huo siku chache baada ya kuathiriwa na ugonjwa wa Uviko 19 ambapo wafanyakazi wa kiwanda hicho walionekana katika video zilizosambaa mtandaoni zikiwaonyesha wafanyakazi wakikimbia kutoka kwenye kiwanda hicho.

Menejimenti ya kiwanda hicho ilitoa notisi tatu siku ya Jumapili wiki iliyopita ikiahidi mpango wa mazingira salama kwa wafanyakazi wake.

Kiwanda hicho, kinachoendeshwa na kikundi cha Teknolojia cha Foxconn cha Taiwan na kinachodaiwa kuwa kituo kikubwa zaidi cha Iphone, kilikuwa kimeweka hatua kali za udhibiti wa ugonjwa huo kwa siku 10 zilizopita.

Sheria hizo zilijumuisha vipimo vya kila siku na marufuku ya kula kwenye kantini ya kiwanda hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!