Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kiwanda cha iphone China chatoa ahadi ya kudhibiti Uviko 19
Habari Mchanganyiko

Kiwanda cha iphone China chatoa ahadi ya kudhibiti Uviko 19

Spread the love

 

KIWANDA cha Iphone cha Zhengzhou, China kimetoa ahadi ya kuhakikisha usalama kwa wafanyakazi walioamua kuondoka na wale watakaobaki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kiwanda hicho kimefikia uamuzi huo siku chache baada ya kuathiriwa na ugonjwa wa Uviko 19 ambapo wafanyakazi wa kiwanda hicho walionekana katika video zilizosambaa mtandaoni zikiwaonyesha wafanyakazi wakikimbia kutoka kwenye kiwanda hicho.

Menejimenti ya kiwanda hicho ilitoa notisi tatu siku ya Jumapili wiki iliyopita ikiahidi mpango wa mazingira salama kwa wafanyakazi wake.

Kiwanda hicho, kinachoendeshwa na kikundi cha Teknolojia cha Foxconn cha Taiwan na kinachodaiwa kuwa kituo kikubwa zaidi cha Iphone, kilikuwa kimeweka hatua kali za udhibiti wa ugonjwa huo kwa siku 10 zilizopita.

Sheria hizo zilijumuisha vipimo vya kila siku na marufuku ya kula kwenye kantini ya kiwanda hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!