Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali ya ndege Bukoba; Samia awataka Watanzania kuwa watulivu
Habari Mchanganyiko

Ajali ya ndege Bukoba; Samia awataka Watanzania kuwa watulivu

Baadhi ya abiria waliokolewa katika ajali ya ndege ya Precision
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amewaasa Watanzania kuwa watulivu wakati zoezi la uokoaji linaendelea katika na ajali ya ndege namba PW 494 ya Kampuni ya Precision Air iliyotokea leo tarehe 6 Novemba, 2022 wilayani Bukoba mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu, Bukoba … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa leo kupitia mtandao wa Twitter, Rais Samia ameandika, “Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali ya ndege ya Shirika la Precision katika Ziwa Victoria, mkoani Kagera.

“Natuma salamu za pole kwa wote walioathirika na ajali hii. Tuendelee kuwa watulivu wakati huu zoezi la uokoaji likiendelea huku tukimuomba Mwenyezi Mungu atusaidie.”

Ndege hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam, kuelekea Bukoba, imepata hitilafu na kulazimika kutua majini mjini Bukoba ikiwa ni umbali unaokadiriwa kuwa mita 100 kutoka ulipo uwanja wa ndege Bukoba.

Taarifa zilizothibitishwa na mmoja wa wafanyakazi wa ndege hiyo zinasema, hitilafu hiyo, ilitokana na ndege hiyo, kushindwa kutoa matairi wakati wa kutua katika uwanja wa Ndege wa Bukoba, majira ya saa tatu asubuhi ya leo Jumapili, 6 Novemba 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!