Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kibano chaja kwa waagizaji magari ‘used’ watakaokwepa ukaguzi Japan
Habari Mchanganyiko

Kibano chaja kwa waagizaji magari ‘used’ watakaokwepa ukaguzi Japan

Sehemu ya magari yakiwa bandarini yakisubiri kutolewa na wamiliki wake
Spread the love

 

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limewataka waagizaji wa magari yaliyotumika kutoka Japan, mawakala wa forodha na wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha wanakagua magari hayo kabla ya kusafirishwa kuja Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 28 Septemba, 2022 na Meneja Uhusiano na Masoko kutoka TBS, Gladness Kaseka imesema watakaoshindwa kukidhi matakwa hayo watakumbana na adhabu.

Imesema Shirika litalazimika kuyakagua magari hayo hapa nchini sambamba na adhabu ya asilimia 30 ya jumla ya gharama ya gari husika na usafiri (Cost and Freight) kwa kuzingatia nyaraka za kodi zilizohakikiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Hayo yanajiri baada ya Shirika hilo kutoa taarifa tarehe 20 Julai, 2022 kwamba magari yote yaliyotumika (used motor vehicles) yanayotoka nchini Japan yatakuwa yanakaguliwa nchini Japan kabla ya kuja Tanzania kwa utaratibu wa Pre-Shipment Verification of Conformity to Standard (PVoC).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!