Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hawa hapa wabunge Afrika Mashariki, Spika Tulia awapa maagizo
Habari za SiasaTangulizi

Hawa hapa wabunge Afrika Mashariki, Spika Tulia awapa maagizo

Angela Kizigha
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson, amewataka wabunge tisa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA), kusimamia maslahi ya Tanzania pamoja na kuwasilisha hoja za nchi badala ya hoja zao binafsi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Spika Tulia ametoa agizo hilo leo Alhamisi, tarehe 22 Septemba 2022, bungeni jijini Dodoma, muda mfupi baada ya Katibu wa Bunge, Nenelwa Mwihambi, kuwatangaza washindi wa uchaguzi wa EALA.

“Wabunge hawa ndiyo wabunge tumewachagua sisi siku ya leo kwa niaba ya wananchi wote kwenda kutuwakilisha kama Tanzania kwenye Bunge la Afrika Mashariki na tunawategemea mnapokwenda kule si hoja ya mawazo yenu, ni hoja ya nchi inasemaje na tunaamini mtaenda kusimamia maslahi ya nchi kama mlivyoahidi hapa,” amesema Spika Tulia.

Dk. Ng’waru Maghembe

Aidha, Spika Tulia amewataka wabunge hao wateule kuzingatia majukumu yao watakayopewa na EALA, pamoja na kutoa mrejesho kwa Bunge la Tanzania juu ya kazi watakazozifanya.

Dk. Abdula Hasnuu Makame,

“Niwape ushauri kama ambavyo sisi huwa tunaenda majimboni kwetu, ninyi jimbo lenu ni hili hapa kwa niaba ya Watanzania. Lakini muhimu kuzingatia kazi zile ambazo mnapaswa kuzifanya huko, huku lazima mtupatie taarifa kwa kazi zenu kwa kadiri ambayo mnatakiwa kufanya hivyo na kanuni,” amesema Spika Tulia.

Wabunge hao wateule ni Angella Kiziga, aliyepata kura 322, zilizopigwa katika kundi  la wagombea wanawake, mwingine katika kundi hilo ni Nadra Juma Mohammed (310), Dk. Shogo Mlozi (322).

Wabunge waliochaguliwa kutoka kundi la wagombea kutoka Zanzibar, ni Abdullah Makame aliyepata kura 305, kati ya kura 311 zilizopigwa na Machano Ally Machano (291).

Mashaka Ngole, kutoka Chama cha Wananchi (CUF), amechaguliwa katika kundi la wagombea wa vyama vya waliowachache bungeni, ambapo amepata kura 234, kati ya kura 319 zilizopigwa.

Angela Kizigha

Kwa upande wa kundi la wagombea wa Tanzania Bara, walioshinda ni Ansar Abubakar Kachwamba, aliyepata kura 300 kati ya kura 313 zilizopigwa. Wengine ni James Kinyasi Millya (312) na Dk. Ngwalu Jumanne Maghembe (311).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!