Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mshukiwa mauaji ya Abe kufanyiwa uchunguzi wa kiakili
Kimataifa

Mshukiwa mauaji ya Abe kufanyiwa uchunguzi wa kiakili

Spread the love

MTU anayetuhumiwa kumuua Waziri Mkuu wa zamani wa Japan, Shinzo Abe anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa hali yake ya kiakili ili kutathmini afya yake ya kiakili wakati wa tukio hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Abe aliuawa kwa kupigwa risasi kwenye kampeni tarehe 8 Julai, 2022 katika mji wa magharibi wa Nara, siku mbili kabla ya uchaguzi wa bunge nchini humo.

Mshukiwa wa muuaji hayo Tetsuya Yamagami mwenye umri wa miaka 41 yuko kizuizini na inasemekana alimlenga Abe kwa kuwa aliamini kiongozi huyo wa zamani alihusishwa na Kanisa la Muungano.

Mahakama ya Wilaya ya Nara iliidhinisha ombi la ofisi ya waendesha mashitaka la kufanyika uchunguzi wa kiakili unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu.

Abe alikuwa mwanasiasa mashuhuri na maarufu zaidi nchini Japan, alijiuzulu mwaka 2020 kutokana na sababu za kiafya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!