Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mshukiwa mauaji ya Abe kufanyiwa uchunguzi wa kiakili
Kimataifa

Mshukiwa mauaji ya Abe kufanyiwa uchunguzi wa kiakili

Spread the love

MTU anayetuhumiwa kumuua Waziri Mkuu wa zamani wa Japan, Shinzo Abe anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa hali yake ya kiakili ili kutathmini afya yake ya kiakili wakati wa tukio hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Abe aliuawa kwa kupigwa risasi kwenye kampeni tarehe 8 Julai, 2022 katika mji wa magharibi wa Nara, siku mbili kabla ya uchaguzi wa bunge nchini humo.

Mshukiwa wa muuaji hayo Tetsuya Yamagami mwenye umri wa miaka 41 yuko kizuizini na inasemekana alimlenga Abe kwa kuwa aliamini kiongozi huyo wa zamani alihusishwa na Kanisa la Muungano.

Mahakama ya Wilaya ya Nara iliidhinisha ombi la ofisi ya waendesha mashitaka la kufanyika uchunguzi wa kiakili unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu.

Abe alikuwa mwanasiasa mashuhuri na maarufu zaidi nchini Japan, alijiuzulu mwaka 2020 kutokana na sababu za kiafya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!