Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari Sri Lanka waandamana kumng’oa rais aliyekaimu
HabariKimataifa

Sri Lanka waandamana kumng’oa rais aliyekaimu

Spread the love

WAANDAMANAJI wamekusanyika katika kituo cha treni mjini Colombo nchini Sri Lanka kutaka kaimu Rais Ranil Wickremesinghe aondoke madarakani.

Ranil aliteuliwa kuwa rais wa muda wa Sri Lanka baada ya Gotabaya Rajapaska kuimbia nchi hiyo na kwenda uhamishoni ambapo alitangaza kujiuzulu kufuatia maandamano ya miezi kadhaa. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea)

Maandamano yamekuwa yakiendelea Sri Lanka baada ya uchumi wa nchi hiyo kuanguka.

Kaimu rais Ranil, alitangaza hali ya dharura na kumpa mamlaka makubwa ya kuongoza nchi hiyo licha ya maandamano kuongezeka kutaka ajiuzulu.

Bunge la Sri Lanka linatarajiwa kumchagua rais mpya katika muda wa siku mbili.

Waandamanaji wamesema kwamba tangazo la hali ya dharura halitawazuia kuendelea kutaka kuundwa kwa serikali mpya.

Maandamano hayo yanaingia siku ya 100, huku zaidi ya watu milioni 22 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, mafuta na dawa tangu mwishoni mwa mwaka uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!