Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Sri Lanka waandamana kumng’oa rais aliyekaimu
HabariKimataifa

Sri Lanka waandamana kumng’oa rais aliyekaimu

Spread the love

WAANDAMANAJI wamekusanyika katika kituo cha treni mjini Colombo nchini Sri Lanka kutaka kaimu Rais Ranil Wickremesinghe aondoke madarakani.

Ranil aliteuliwa kuwa rais wa muda wa Sri Lanka baada ya Gotabaya Rajapaska kuimbia nchi hiyo na kwenda uhamishoni ambapo alitangaza kujiuzulu kufuatia maandamano ya miezi kadhaa. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea)

Maandamano yamekuwa yakiendelea Sri Lanka baada ya uchumi wa nchi hiyo kuanguka.

Kaimu rais Ranil, alitangaza hali ya dharura na kumpa mamlaka makubwa ya kuongoza nchi hiyo licha ya maandamano kuongezeka kutaka ajiuzulu.

Bunge la Sri Lanka linatarajiwa kumchagua rais mpya katika muda wa siku mbili.

Waandamanaji wamesema kwamba tangazo la hali ya dharura halitawazuia kuendelea kutaka kuundwa kwa serikali mpya.

Maandamano hayo yanaingia siku ya 100, huku zaidi ya watu milioni 22 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, mafuta na dawa tangu mwishoni mwa mwaka uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!