Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari Biashara Mbeya Kwanza zaaga Ligi Kuu
HabariMichezo

Biashara Mbeya Kwanza zaaga Ligi Kuu

Spread the love

 

Klabu ya soka ya Biashara United ya mkoani Mara rasmi imeshuka daraja na kuungana na Mbaya Kwanza iliyokua ishashuka daraja tayari baada ya Biashara kukubali kichapo cha mabao 4-1 kutoka kwa Azam Fc leo 29 juni 2022 katika dimba la Azam Complex jijini Dar es salaam na hivyo kujikatia tiketi ya kucheza Championship msimu ujao. Anaripoti Damas Ndelema Tudarco ….. (endelea)

Biashara ambao walikua na kiwango bora msimu uliopita na kumaliza kuafanikiwa kukamata nafasi ya nne kwenye msimamo na kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa wanashuka daraja wakiwa wamekusanya pointi 28 katika michezo 30.

Timu hiyo inashika  nafasi ya pili kutoka mkiani hivyo kuungana na Mbeya kwanza ambaye leo kapata suluhu ya bila kufungana na Simba katika uwanja wa majimaji Songea hivyo watashuka moja kwa moja hadi Champioship ambapo Biashara wamekaa ligi kuu kwa zaidi ya miaka mitatu, Mbeya kwanza wao wamekaa msimu mmoja tu wamepanda na kushuka daraja

Aidha klabu ya Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons watacheza mechi ya play off ambapo mshindi ataenda kucheza na klabu ya JKT Tanzania ili kupata timu kukamilisha timu kumi na tano za msimu ujao na atakae poteza basi atakwenda Championship msimu ujao

Aidha klabu za Mbeya kwanza na Biashara United hazijashuka kinyonge kwani kila mmoja amejikulia kitita cha shilingi millioni kumi kutoka kwa wadhamini wa ligi na bonasi kutoka kwa Azam Tv , pia watapishana na Singinda Big stars pamoja na Ihefu Fc ambazo zimepanda msimu huu zikitokea Championship

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!