Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya kina Mdee kusikilizwa siku 14 mfululizo
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya kina Mdee kusikilizwa siku 14 mfululizo

Spread the love

 

HATIMA ya endapo Halima Mdee na wenzake 18 wataendelea kusalia kuwa wabunge itajulikana ndani ya siku 14 za usikilizaji wa shauri namba 27 la mwaka 2022. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Shauri hilo linalosikilizwa na Jaji Mustapha Ismail katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam limefunguliwa na Halima Mdee na wenzake 18 dhidi ya Bodi ya wadhamini ya Chadema, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Halima na wenzake wanapinga kuvuliwa uanachama wa chama hicho mara baada ya Baraza Kuu la chama hicho kubariki uamuzi wa Kamati Kuu ya kuwafukuza uanachama kwa makosa ya usaliti.

Leo Alhamisi tarehe 29 Juni, 2022, Mahakama hiyo imetoa kibali kwa wajibu maombi wote kuwasilisha viapo kinzani kesho Alhamisi tarehe 30 Juni, 2022 tayari kwa kuanza kusikiliza shauri hilo.

Hatua hiyo imejiri baada ya Kibatala kuiomba Mahakama hiyo kuondosha mapingamizi waliyowasilisha awali ili kupisha usikilizwaji wa shauri hilo kwa kuwa limefunguliwa mahakamani hapo kwa Hati ya dharura.

Jaji Mustapha Ismail amekubali ombi hilo na kuamua kuondoa mapingamizi hayo kabla ya shauri la msingi kuendelea kusikilizwa ambapo amesema kuwa amri ya zuio itaendelea mpaka shauri la msingi litakapofika mwisho.

“Baada ya kusikiliza hoja za Mawakili nimeamua Hati ya mapingamizi ya awali inaondolewa mapingamizi yote hayatataendelea”

Pia Jaji Mustapha amesema kuwa amri ya itaendelea mpaka mwisho wa shauri la msingi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!