Klabu ya soka ya Biashara United ya mkoani Mara rasmi imeshuka daraja na kuungana na Mbaya Kwanza iliyokua ishashuka daraja tayari baada ya Biashara kukubali kichapo cha mabao 4-1 kutoka kwa Azam Fc leo 29 juni 2022 katika dimba la Azam Complex jijini Dar es salaam na hivyo kujikatia tiketi ya kucheza Championship msimu ujao. Anaripoti Damas Ndelema Tudarco ….. (endelea)
Biashara ambao walikua na kiwango bora msimu uliopita na kumaliza kuafanikiwa kukamata nafasi ya nne kwenye msimamo na kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa wanashuka daraja wakiwa wamekusanya pointi 28 katika michezo 30.
Timu hiyo inashika nafasi ya pili kutoka mkiani hivyo kuungana na Mbeya kwanza ambaye leo kapata suluhu ya bila kufungana na Simba katika uwanja wa majimaji Songea hivyo watashuka moja kwa moja hadi Champioship ambapo Biashara wamekaa ligi kuu kwa zaidi ya miaka mitatu, Mbeya kwanza wao wamekaa msimu mmoja tu wamepanda na kushuka daraja
Aidha klabu ya Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons watacheza mechi ya play off ambapo mshindi ataenda kucheza na klabu ya JKT Tanzania ili kupata timu kukamilisha timu kumi na tano za msimu ujao na atakae poteza basi atakwenda Championship msimu ujao
Aidha klabu za Mbeya kwanza na Biashara United hazijashuka kinyonge kwani kila mmoja amejikulia kitita cha shilingi millioni kumi kutoka kwa wadhamini wa ligi na bonasi kutoka kwa Azam Tv , pia watapishana na Singinda Big stars pamoja na Ihefu Fc ambazo zimepanda msimu huu zikitokea Championship
Leave a comment