Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani kuipa Ukraine makombora ya masafa marefu vita na Urusi
Kimataifa

Marekani kuipa Ukraine makombora ya masafa marefu vita na Urusi

Spread the love

MAREKANI itaitumia Ukraine mifumo ya juu zaidi ya roketi kuisaidia kujilinda, Rais Biden ametangaza.

Kwa mujibu wa BBC silaha hizo, zilizoombwa kwa muda mrefu na Ukraine, ni kusaidia kushambulia vikosi vya adui kwa usahihi kutoka umbali mrefu.

Hadi sasa, Marekani ilikuwa imekataa ombi hilo kwa kuhofia silaha hizo zinaweza kutumika dhidi ya shabaha nchini Urusi.

Lakini siku ya Jumatano, Bw Biden alisema msaada huo utaimarisha msimamo wa Kyiv wa mazungumzo dhidi ya Urusi na kuleta suluhu la kidiplomasia zaidi.

Akiandika katika gazeti la New York Times, alisema: “Ndiyo maana nimeamua kuwa tutawapa Waukraine mifumo ya juu zaidi ya roketi na zana ambazo zitawawezesha kushambulia kwa usahihi shabaha muhimu kwenye uwanja wa vita nchini Ukraine.”

Silaha mpya zitajumuisha Mfumo wa Roketi wa Kivita wa M142 (HIMARS), afisa mkuu wa Ikulu ya White House alisema – ingawa hakufafanua ni ngapi kati yao zitatolewa.

Mifumo hiyo inaweza kurusha makombora mengi ya kuongozwa kwa usahihi katika shabaha hadi kilomita 70 (maili 45) – mbali zaidi kuliko mizinga ambayo Ukraine inayo sasa hivi. Pia inaaminika kuwa sahihi zaidi kuliko silaha za Urusi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!