Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika afafanua uamuzi wake kutowafukuza Mdee, wenzake bungeni
Habari za Siasa

Spika afafanua uamuzi wake kutowafukuza Mdee, wenzake bungeni

Spread the love

 

Spika wa Bunge la Tanzania Dk.Tulia Akson, ametoa ufafanuzi zaidi kuhusu uamuzi wake wa kutowafukuza bungeni wabunge 19 wa Chadema baada ya kupokea barua kutoka kwa chama hicho kumjulisha kuwa wabunge hao si wanachama wa chama hicho. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Dk. Tulia amelazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya mjadala mkali kuibuka kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uamuzi wake huo alioutoa asubuhi.

Baaadhi ya watu walihoji kwanini Spika ajizuie kufanya maamuzi kabla hata ya zuio la Mahakama kutolewa juu ya maombi ya wabunge 19.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu tarehe 16 Mei, 2022, Dk. Tulia amesema amechukua uamuzi huo mara tuu baada ya kujulishwa kuhusu uwepo wa kesi na yeye mwenyewe kujiridhisha.

Amefafanua zaidi kuwa Katiba inaeleza kuwa Mahakama ndiyo chombo cha mwisho cha uamuzi ikiwa mbunge ni halali au la.

Spika wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson

Amesema kwa kutambua hivyo mara baada ya kufahamu kuwa kuna kesi juu ya uhalali wa wabunge hao hawezi kuwafukuza hadi hapo mahakama itakapotoa uamuzi wa kesi hiyo.

“Kwa mbunge ambaye amefuata taratibu zote za kuapishwa na akawa mbunge bila kujali ni wajimbo au Viti Maalumu anapokuwa amefukuzwa ubunge na kwenda kufungua kesi mahakamani anaendelea kuwa na sifa hadi hapo mahakama itakapokuwa imetoa amri.

“Mimi kazi yangu ni kutangaza na mahakama itakapotamka kuwa hawana sifa ya kuwa wabunge, mimi nitatangaza n ahata wasingeenda mahakamani kupinga ningetangaza kwamba nafasi zipo wazi,” amesema.

Alipoulizwa juu ya wabunge wa CUF ambao walifukuzwa ubunge huku kesi ikiendelea hadi leo amesema kuwa “naomba tujielekeze kwa yaliyotukia sasa kwasababu muda ni mchache.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!