Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Mazungumzo yaanza kuwaondoa wanajeshi waliojeruhiwa Mariupol
HabariKimataifa

Mazungumzo yaanza kuwaondoa wanajeshi waliojeruhiwa Mariupol

Spread the love

RAIS wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amesema kuwa wanafanya kila wawezalo kuhakikisha wanawaondosha wanajeshi wao, waliojeruhiwa katika jimbo la Mariupol. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa mitandao … (endelea).

Ikumbukwe kwamba Urusi inataka kuchukua udhibiti wa mji wa Mariupol ambao wamekuwa wakiupigania kwa makombora kwa miezi kadhaa sasa.

Zelensky ametoa kauli hiyo, katika matangazo ya kila wiki ambayo amekuwa akiyatoa tangu kkuanza kwa uvamizi wa Urusi dhidi ya nchi yake.

Wakati huohuo, vikosi vya Ukraine vilivyopo karibu na Mariupol vilijificha katika kiwanda cha chuma wakati vikosi vya Urusi vilipowashambulia.

Hata hivyo, jeshi limetoa wito wa msaada baada ya wanajeshi wengi kujeruhiwa,’’ hapakuwa nan jia ambayo wangeweza kuitumia ili kutoroka katika eneo hilo, kwasababu jeshi la Urusi lilikuwa limezingira eneo hilo.’’

Katika hotuba ya Rais Zelensky, amesema kuwa wameanza mazungumzo ya kuangalia iwapo kama vikosi vya Urusi vitaruhusu kuwaondoa majeruhi.

Lakini Zelensky ameongeza kuwa mazungumzo hayo nimagumu sana.

Aidha hakuwataja wawakilishi wa Ukraine katika mazungumzo hayo, lakini amesema ni wao waliotaka yaanzishwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!