Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamati yaomba miradi ya maendeleo iliyozuiwa kurudishwa Ngorongoro
Habari Mchanganyiko

Kamati yaomba miradi ya maendeleo iliyozuiwa kurudishwa Ngorongoro

Spread the love

KAMATI ya kukusanya mapendekezo ya wananchi na wadau juu ya kumaliza mgogoro wa ardhi katika Hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha, imeiomba Serikali irudishe miradi ya maendeleo na huduma za kijamii, zilizozuiliwa kwenda wilayani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Ombi hilo limetolewa leo Jumatatu, tarehe 25 Aprili 2022, mkoani Arusha, katika kikao cha siku mbili cha kamati hiyo, cha ukamilishaji mchakato wa ukusanyaji maoni na mapendekezo, ambayo yatawasilishwa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wiki hii.

“Serikali irudishe miradi yote ya maendeleo na huduma za jamii zilizozuiliwa kwenda Tarafa ya Ngorongoro,” imesema taarifa ya kamati hiyo.

Wito huo umetolewa ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Ngorongoro, Dk. Jumaa Mhina, kuwaagiza wakuu wa Shule za Msingi nne wilayani humo, kuhamisha kiasi cha Sh. 160 milioni, zilizopelekwa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, katika Wilaya ya Handeni.

Aidha, kamati hiyo imeiomba Serikali isitishe mipango yote inayoendelea kuhusu mgogoro huo unaodaiwa kuibuka kufuatia ongezeko la idadi ya watu kwenye Hifadhi ya Ngorongoro, hadi pale maoni ya wananchi watakapofanyiwa kazi.

Kwa mujibu wa taarifa ya kamati hiyo, mchakato wa uchukuaji maoni na mapendekezo ya utatuzi wa mgogoro huo, umekamilika.

“Mchakato wa kukusanya maoni ya wananchi kwa vijjji vyote vinavyozunguka eneo lenye mgogoro wa kilometa za mraba 1500 na eneo la mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, umekamilika kama tulivyoeleza awali na taarifa ya maoni hayo inatarajiwa kuwasilishwa kwa Waziri Majaliwa, pamoja na viongozi wa juu wa Serikali pamoja na umma,” imesema taarifa hiyo.

Kamati hiyo yenye wajumbe kutoka makundi mbalimbali, inajumuisha watu 60 kutoka kata za Loliondo, Sale na Ngorongoro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!