Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Biashara Wenye viwanda watakiwa kuacha urasimu utoaji bidhaa
Biashara

Wenye viwanda watakiwa kuacha urasimu utoaji bidhaa

Spread the love

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji amewataka wamiliki wa viwanda vya saruji na sukari kupunguza urasimu katika utoaji wa bidhaa hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Kijaji ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam leo tarehe 11 Aprili wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa nchini.

Amesema urasimu huo unasababisha upungufu wa bidhaa kwenye soko na kufanya bei kuongezeka pasipo sababu za msingi.

Amesema baada ya kukutana na wadau wa sekta hizo bei hizo zimeshuka ikilinganishwa na nchi zingine za Afrika Mashariki.

Amesema bei ya saruji imepungua kutoka Sh 17,000 kwa mfuko mmoja wa kilo 50 hadi Sh 16, 125 kwa bei za mwezi Machi.

Aidha, amesema bei ya sukari nayo imepungua hadi kufikia Sh 2,670 kutoka Sh 3,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

Biashara

Promosheni ya bil 1 kutoka Meridianbet kasino, cheza na ushinde zawadi kubwa

Spread the love  INGIA katika ulimwengu wa zawadi za kushangaza: Jishindie sehemu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

error: Content is protected !!