Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Biashara Wenye viwanda watakiwa kuacha urasimu utoaji bidhaa
Biashara

Wenye viwanda watakiwa kuacha urasimu utoaji bidhaa

Spread the love

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji amewataka wamiliki wa viwanda vya saruji na sukari kupunguza urasimu katika utoaji wa bidhaa hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Kijaji ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam leo tarehe 11 Aprili wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa bei za bidhaa nchini.

Amesema urasimu huo unasababisha upungufu wa bidhaa kwenye soko na kufanya bei kuongezeka pasipo sababu za msingi.

Amesema baada ya kukutana na wadau wa sekta hizo bei hizo zimeshuka ikilinganishwa na nchi zingine za Afrika Mashariki.

Amesema bei ya saruji imepungua kutoka Sh 17,000 kwa mfuko mmoja wa kilo 50 hadi Sh 16, 125 kwa bei za mwezi Machi.

Aidha, amesema bei ya sukari nayo imepungua hadi kufikia Sh 2,670 kutoka Sh 3,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Biashara

Black Gold kasino mgodi wa madini Meridianbet 

Spread the love  Dhahabu ni moja kati ya utajiri wenye thamani kubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!