Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kakoso: Bandari Karema haina maana bila reli, barabara
Habari za Siasa

Kakoso: Bandari Karema haina maana bila reli, barabara

Spread the love

MBUNGE wa Mpanda Vijijini, Selemani Kakoso (CCM) amesema mradi wa wa ujnenzi wa Bandari ya Karema katika Ziwa Tanganyika hautakuwa na maana kama hautaunganishwa na reli na barabara nzuri. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Ameyasema hayo leo Jumatatu ya terehe 11 Aprili, 2022 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akichangia hoja bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake .

Kakoso ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu amesema ni vyema unejzi wa bandari hiyo kwenda sambamba na ujenzi wa reli kutoka Kaliua-Mpanda hadi Karema.

Amesema pia lazima kuwe na mpango uwekezaji katika ujenzi wa barabara ya Kabungu hadi Karema ili kuiunganisha bandari hiyo na bandari ya Dar es Salaam.

“Tunayo fursa ambayo tunaweza kuipata Serikali ikiwekeza inavyopaswa. Sisi kama nchi ni vyema tukawa na uwekezaji mkubwa ili wananchi wanufaike.

“Tujipange kuahakikisha nchi ya DRC ambayo imejiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, inatumia ile bandari na ikunganishwa na matawi ya reli na barabara tuna fursa kubwa ya bandari ya Dar es Salaam kupata mzigo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!