MBUNGE wa Bukoba Vijijini, Dk. Jasson Rweikiza ameishauri Serikali kuanzisha utaratibu wa kilimo cha makambi ili kuongeza uzalishaji mali na ajira kwa vijana. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Dk. Rweikiza ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 11 Aprili, 2022, bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake.
Amesema kupitia makambi hayo Serikali itoe mikopo itakayowawezesha kujenga kambi, kununua trekta, na pembejeo zingine za kilimo.
“Mfano tukianzisha kambi za vijana 200, wapewe hekari 2000 na mkopo wa milioni 200 waanze na mazao ya muda mfupi mfano maharage, mahindi, alizeti n.k baadaya miezi mitatu watapata mazao mengi na watauza nje,” amesema.
Amesema baada ya mwaka mmoja kama watakuwa wanafanya kilimo cha umwagiliaji, wataweza kurejesha mkopo wao na wataendelea na uzalishaji, “wanaweza wakajilipa mishahara ya milioni moja kila mwezi na tukaondokana na tatizo la ajira.”
Leave a comment