Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aitaka Serikali ianzishe kilimo cha makambi
Habari za Siasa

Mbunge aitaka Serikali ianzishe kilimo cha makambi

Spread the love

MBUNGE wa Bukoba Vijijini, Dk. Jasson Rweikiza ameishauri Serikali kuanzisha utaratibu wa kilimo cha makambi ili kuongeza uzalishaji mali na ajira kwa vijana. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Rweikiza ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 11 Aprili, 2022, bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake.

Amesema kupitia makambi hayo Serikali itoe mikopo itakayowawezesha kujenga kambi, kununua trekta, na pembejeo zingine za kilimo.

“Mfano tukianzisha kambi za vijana 200, wapewe hekari 2000 na mkopo wa milioni 200 waanze na mazao ya muda mfupi mfano maharage, mahindi, alizeti n.k baadaya miezi mitatu watapata mazao mengi na watauza nje,” amesema.

Amesema baada ya mwaka mmoja kama watakuwa wanafanya kilimo cha umwagiliaji, wataweza kurejesha mkopo wao na wataendelea na uzalishaji, “wanaweza wakajilipa mishahara ya milioni moja kila mwezi na tukaondokana na tatizo la ajira.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!