MBUNGE wa Kawe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Askofu Joseph Gwajima ameshauri kuanzishwa kwa Dira ya Taifa ili kuwezesha kiongozi yoyote anayeingia madarakani asitumie mawazo yake peke yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Gwajima ambaye ni Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, amesema hayo leo Jumatatu tarehe 11 Aprili 2022, bungeni jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Fungu la Bunge kwa mwaka 2022/23.
Askofu Gwajima amesema, bila kuwa na dira ya Taifa, “ipo siku, kama tutaruhusu anayeingia madarakani aongozwe na kichwa chake, ipo siku tutapata Rais wa ajabu.”
Fuatilia mchango wote wa Askofu Gwajima kupitia MwanaHALISI TV
Asante ndugu