MBUNGE wa Mpanda Vijijini, Selemani Kakoso (CCM) amesema mradi wa wa ujnenzi wa Bandari ya Karema katika Ziwa Tanganyika hautakuwa na maana kama hautaunganishwa na reli na barabara nzuri. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Ameyasema hayo leo Jumatatu ya terehe 11 Aprili, 2022 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akichangia hoja bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake .
Kakoso ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu amesema ni vyema unejzi wa bandari hiyo kwenda sambamba na ujenzi wa reli kutoka Kaliua-Mpanda hadi Karema.
Amesema pia lazima kuwe na mpango uwekezaji katika ujenzi wa barabara ya Kabungu hadi Karema ili kuiunganisha bandari hiyo na bandari ya Dar es Salaam.
“Tunayo fursa ambayo tunaweza kuipata Serikali ikiwekeza inavyopaswa. Sisi kama nchi ni vyema tukawa na uwekezaji mkubwa ili wananchi wanufaike.
“Tujipange kuahakikisha nchi ya DRC ambayo imejiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki, inatumia ile bandari na ikunganishwa na matawi ya reli na barabara tuna fursa kubwa ya bandari ya Dar es Salaam kupata mzigo.”
Leave a comment