Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aitaka Serikali ianzishe kilimo cha makambi
Habari za Siasa

Mbunge aitaka Serikali ianzishe kilimo cha makambi

Spread the love

MBUNGE wa Bukoba Vijijini, Dk. Jasson Rweikiza ameishauri Serikali kuanzisha utaratibu wa kilimo cha makambi ili kuongeza uzalishaji mali na ajira kwa vijana. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Rweikiza ametoa wito huo leo Jumatatu tarehe 11 Aprili, 2022, bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hoja ya hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara zake.

Amesema kupitia makambi hayo Serikali itoe mikopo itakayowawezesha kujenga kambi, kununua trekta, na pembejeo zingine za kilimo.

“Mfano tukianzisha kambi za vijana 200, wapewe hekari 2000 na mkopo wa milioni 200 waanze na mazao ya muda mfupi mfano maharage, mahindi, alizeti n.k baadaya miezi mitatu watapata mazao mengi na watauza nje,” amesema.

Amesema baada ya mwaka mmoja kama watakuwa wanafanya kilimo cha umwagiliaji, wataweza kurejesha mkopo wao na wataendelea na uzalishaji, “wanaweza wakajilipa mishahara ya milioni moja kila mwezi na tukaondokana na tatizo la ajira.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!